KITUO CHA SITA



 KITUO CHA SITA 

VERONIKA ANAUPANGUSA USO WA YESU

P. Hapo, hao watu wema watamjibu mfalme: "Bwana, lini tulikuona mwenye njaa tukakupa chakula, au ukiwa na kiu tukakunywesha maji? Lini tulikuona ukiwa mgeni tukakukaribisha au bila nguo tukakuvika? Lini tulikuona ukiwa mgonjwa tukaja kukutazama?” Mfalme atawajibu: “Kweli nawaambieni, kila kitu mlichomtendea mmojawapo wa hawa ndugu zangu wadogo, mlinitendea mimi" (Mt 25:37-40).

W. Walakini rafiki aliye amini ndiye ngome; naye aliyempata amepata tunu. Hakuna badala ya rafiki amini, wala uzuri wake hauna bei. Rafiki amini ni kifunga uzima; naye amchaye Mungu atampata. Mcha Mungu hunyoosha urafiki wake, kwa maana alivyo yeye mwenyewe, ndivyo alivyo na jirani yake
(YbS 6:14-17).

Tuombe: Yesu, tufanye tuone uso wako ndani ya wanaoteseka. Katika mateso utufundishe upendo, utufundishe upendo hasa katika mateso. Amina


Comments

Popular posts from this blog

NJIA YA MSALABA KATIKA BIBLIA

NJIA YA MSALABA

KITUO CHA KWANZA