KITUO CHA SITA
KITUO CHA SITA
VERONIKA ANAUPANGUSA USO WA YESU
P. Hapo, hao watu wema watamjibu mfalme: "Bwana, lini tulikuona mwenye njaa tukakupa chakula, au ukiwa na kiu tukakunywesha maji? Lini tulikuona ukiwa mgeni tukakukaribisha au bila nguo tukakuvika? Lini tulikuona ukiwa mgonjwa tukaja kukutazama?” Mfalme atawajibu: “Kweli nawaambieni, kila kitu mlichomtendea mmojawapo wa hawa ndugu zangu wadogo, mlinitendea mimi" (Mt 25:37-40).W. Walakini rafiki aliye amini ndiye ngome; naye aliyempata amepata tunu. Hakuna badala ya rafiki amini, wala uzuri wake hauna bei. Rafiki amini ni kifunga uzima; naye amchaye Mungu atampata. Mcha Mungu hunyoosha urafiki wake, kwa maana alivyo yeye mwenyewe, ndivyo alivyo na jirani yake
(YbS 6:14-17).
Tuombe: Yesu, tufanye tuone uso wako ndani ya wanaoteseka. Katika mateso utufundishe upendo, utufundishe upendo hasa katika mateso. Amina

Comments
Post a Comment