KITUO CHA KWANZA

KITUO CHA KWANZA 

 YESU ANAHUKUMIWA AFE

P: Kuhani Mkuu akamwuliza tena. "Je, wewe ndiye Masiha, Mwana wa Mungu Mtukufu?” Yesu akajibu, "Naam, mimi ndiye. Tena, mtamwona Mwana wa Mtu amekaa upande wa kulia wa Mwenye Nguvu, akija katika mawingu ya mbinguni”. Hapo Kuhani Mkuu akararua joho lake, akasema, Tuna haja gani tena ya mashahidi? Mmesikia kufuru yake! Ninyi mwaonaje?” Wote wakamua kwamba anastahili kuuawa. (Mk 14:61-64).

W: Wafalme wa dunia wanajipanga, Na wakuu wanafanya shauri pamoja, juu ya Bwana na juu ya Masiha wake, Nitaihubiri amri; Bwana aliniambia, Ndiwe mwanangu, Mimi leo nimekuzaa. Uniombe, nami nitakupa mataifa kuwa urithi wako na miisho ya dunia kuwa milki yako. (Zab 2:7-8).

Tuombe: Mwanakondoo wa Mungu uondoaye dhambi za dunia kwa kutamka kuwa wewe ni Mwana wa Mungu umehukumiwa kufa bila kosa. Tufanye tusikuhukumu mara nyingine kufa kwa dhambi zetu bali kutokana na kifo chako tujaliwe ujasiri wa kukukiri wewe unayekaa upande wa Mwenye-enzi na kutawala daima na milele. Amina






Comments

Popular posts from this blog

NJIA YA MSALABA KATIKA BIBLIA

NJIA YA MSALABA