NJIA YA MSALABA KATIKA BIBLIA

  NJIA YA MSALABA KATIKA BIBLIA


Kabla ya kila kituo:

K: Ee Yesu tunakuabudu, tunakushukuru;
W: Kwa kuwa umewakomboa watu kwa msalaba wako mtakatifu.

Baada ya kila kituo:
'Baba Yetu, 'Salamu Maria' na 'Atukuzwe Baba',
K: Ee Bwana utuhurumie! W: Utuhurumie!
K: Roho za waamini marehemu, wapate rehema kwa Mungu, wapumzike kwa amani. W: Amina

(Kutoka “NJIA YA MSALABA INAYAGOMBEA KATIKA BIBLIA” - kimetungwa na Pdr. Thadei A. Mworia, OSS (Tabora, Tanzania)

SALA YA KUFUNGUA
Yesu akaenda pamoja na wanafunzi wake bustanini Gethsemane, akawaambia, "Kaeni hapa nami niendc pale mbele kusali". Akawachukua Petra na wana wawil wa Zebedayo, akaanza kuwa na huzuni na mahangaiko Hapo akawaambia, “'Nina huzuni kubwa moyoni hate karibu ya kufa. Kaeni hapa mkeshe pamoja nami". Basi, akaenda mbele kidogo, akaanguka kifudifudi akasali, "Baba yangu, kama inawezekana, kikombe hiki cha mateso kinipitie; lakini isiwe nitakavyo mimi, ila utakavyo wewe". (Mt 26:36-39).

Mungu Baba Mwenyezi, pokea sala yetu ya shukrani tuitoayo kwa Mwanao mpendwa, Mwokozi na Bwana wetu. Tunapoyakumbuka mateso yake matakatifu, peleka Roho wako Mtakatifu mioyoni mwetu ili tusalipo au tufanyapo kazi, yote tuyafanye tumeunganika na Kristo Mkombozi wetu, anayeishi na kutawala daima na milele. Amina.

Comments

Popular posts from this blog

NJIA YA MSALABA

KITUO CHA KWANZA