KITUO CHA NANE

 KITUO CHA NANE 

 AKINA MAMA WANAMLILIA YESU

P. Watu, umati kwa umati, walimfuata; miongoni mwao vakiwamo wanawake waliokuwa wanaomboleza na kumlilia. Yesu akawageukia, akasema, "Enyi akina mama wa Yerusalemu! Msinililie mimi, ila lieni kwa ajili yenu wenyewe na kwa ajili ya watoto wenu (Lk 23:27-28).

W. Je si kitu kwenu, enyi nyote mpitao njia, Angalieni, mtazame kama kuna majonzi yoyote mfano wa majonzi yangu, Niliyotendwa mimi, ambayo Bwana amenihuzunisha kwa hayo. Siku za hasira yake iwakayo. Mimi ninayalilia mambo hayo; Jicho langu, jicho langu linachuruzika maji; kwa kuwa mfariji yu mbali nami, ambayo ilimpasa kunihuisha nafsi; Watoto wangu wameachwa poke yao, kwa sababu huyo adui ameshinda (Omb 1:12-16).

Tuombe: Bwana Yesu, hawa wanawake wa Yerusalemu waliodondosha machozi ya huruma walipokuona njiani kwenda Kalvari umepigwa, umechubuliwa, umetobolewa na miiba. Ongeza imani yangu ili niweze kukuona katika ndugu yangu aliyepigwa kwa maneno yangu mabaya, aliyechubuliwa kwa wivu wangu, aliyetobolewa kwa kumkosea haki. Amina

Comments

Popular posts from this blog

NJIA YA MSALABA KATIKA BIBLIA

NJIA YA MSALABA

KITUO CHA KWANZA