KITUO CHA KUMI

 KITUO CHA KUMI 

YESU ANAVULIWA NGUO

P. Nao askari walipomsulibisha Yesu wakampa kunywa divai iliyochanganywa na nyongo; lakini yeye alipoionja hakutaka kunywa... Walitwaa mavazi yake, wakafanya mafungu manne, kwa kila askari fungu lake; na kanzu nayo. Basi kanzu ile haikushonwa, ilikuwa imefumwa yote pia tangu juu. Basi wakaambiana, ‘tusiipasue, lakini tuipigie kura, iwe ya nani’. Ili litimie andiko lile linenalo, waligawana nguo zangu, na vazi langu wakalipigia kura. Basi ndivyo walivyofanya wale askari (Mt 27:34; Yn 19:23-24).

W. Laumu imenivunja moyo, nami ninaugua sana. Nikangoja aje wa kunihurumia, wala hakuna;
Na wa kunifariji, wala sikumwona mtu. Wakanipa uchungu kuwa chakula changu: nami nilipokuwa na kiu wakaninywesha siki. Wao wananitazama na kunikodolea macho. Wanagawanya nguo zangu na vazi langu wanalipigia kura. Nawe Bwana. usiwe mbali, Ee nguvu zangu, fanya haraka kunisaidia (Zab 69:20-21; 22:17-19).

Tuombe: Bwana unavuliwa nguo na kutoneshwa madonda yako. Tupe, tunakuomba, ujasiri wa kuvua cho chote kisichostahili kuvaa juu ya ile nguo nyeupe ya ubatizo ambayo ulitustahilia kwa gharama kubwa namna hiyo. Amina

Comments

Popular posts from this blog

NJIA YA MSALABA KATIKA BIBLIA

NJIA YA MSALABA

KITUO CHA KWANZA