KITUO CHA KUMI NA TATU

 KITUO CHA KUMI NA TATU 

YESU ANASHUSHWA MSALABANI

P: Lakini walipomfikia Yesu waliona kwamba alikwisha kufa, na hivyo hawakumvunja miguu. Lakini askari mmoja akamtoboa ubavuni kwa mkuki na mara ikatoka damu na maji. Baada ya hayo, Yosefu, mwenyeji wa Arimataya, alimuomba Pilato ruhusa ya kuuchukua mwili wa Yesu. Basi Pilato akaamuru apawa (Yn 19:33-34,38; Mt 27:58).

W. Basi tabiri uwaambie, Bwana Mungu asema hivi: Tazama, nitafunua makaburi yenu, na kuwapandisha kutoka katika makaburi yenu, enyi watu wangu, nami nitawaingizeni katika nchi ya Waisraeli. Nanyi mtajua kuwa mimi ndimi Bwana, nitakapoyafunua makaburi yenu na kuwatoa katika makaburi, enyi watu wangu, nami nitatia roho yangu ndani yenu, nanyi mtaishi, nami nitawawekeni katika nchi yenu, nanyi mtajua ya kuwa mimi, Bwana, nimesema hayo, na kuyatimiza asema Bwana. (Eze 37:12-14).

Tuombe: Ee Yesu, ulimrudishia Baba yako wa mbinguni kila alichokupa. Nasi ukatupa kila kitu ulichokuwa nacho, hadi ukatoa uzima wako kwa ajili yetu. Kwa fumbo la sakramenti ya ubatizo na Ekaristi umetufanya wana wa Mungu. Kwa nguvu ya sakramenti hizi tujalie tuweze kujitoa kabisa kwa ajili ya kazi ya kueneza ufalme wa Mungu hapa duniani tukifuata mfano wako wa kujitoa kabisa. Amina.

Comments

Popular posts from this blog

NJIA YA MSALABA KATIKA BIBLIA

NJIA YA MSALABA

KITUO CHA KWANZA