KITUO CHA KUMI NA MOJA


KITUO CHA KUMI NA MOJA

YESU ANASULUBISHWA MSALABANI

P. Walipofika mahali palipoitwa, "Fuvu la Kichwa", ndipo wakamsulubisha Yesu pamoja na wale wahalifu wawili mmoja upande wa kulia na mwingine upande wa kushoto. Yesu akasema, ‘Baba uwasamehe kwani hawajui wanalofanya’. Yesu akalia kwa sauti kubwa akisema, "Eloi Eloi, lema Sabakthani?" maana yake, ‘Mungu wangu, Mungu wangu, mbona umeniacha?" (Lk 23:33-34; Mk 15:34).

W. Mungu wangu, Mungu wangu, Mbona umeniacha? Mbona U mbali na wokovu wangu, na maneno ya kuugua kwangu? Ee Mungu wangu, nalia mchana lakini hujibu, na wakati wa usiku lakini sipati raha. Lakini mimi ni mdudu wala si mtu. Laumu ya wanadamu na mzaha wa watu. Wote wanionao hunicheka sana, hunifyonya, wakitikisa vichwa vyao; Husema amemtegemea Bwana; na amponye, na amwokoe sasa, maana amependwa naye. Nguvu zangu zimekauka kama gae, Ulimi wangu waambatana na taya zangu; unaniweka katika mavumbi ya mauti. Kwa maana mbwa wamenizunguka; Kusanyiko la waovu wamenisonga; wamenitoboa mikono na miguu. Naweza kuihesabu mifupa yangu yote (Zab 22:1-2; 4:6-8,15-17).

Tuombe: Bwana na mkombozi, umetuambia kuwa sharti tukubali kusulubiwa kama tunataka kupata ufufuko. Tusaidie tufurahie mateso yanayotokana na kutimiza wajibu wetu wa kila siku, tuyaone kama njia kuu ya kuufiki ufufuko wetu. Amina

Comments

Popular posts from this blog

NJIA YA MSALABA KATIKA BIBLIA

NJIA YA MSALABA

KITUO CHA KWANZA