KITUO CHA KUMI NA MBILI -
KITUO CHA KUMI NA MBILI
YESU ANAKUFA MSALABANI
P. Ilikuwa yapata saa sita mchana; jua likaacha kuangaza, giza likaivamia nchi yote mpaka saa tisa, na pazia lililokuwa limetundikwa Hekaluni likapasuka katikati. Yesu akalia kwa sauti kubwa: “Baba, mikononi nwako naiweka roho yangu”. Alipokwisha kusema hayo, akatoa roho. Jemadari na wale waliokuwa wakimchunga Yesu walipoona mtetemeko wa ardhi na yale mambo yaliyotukia, wakaogopa sana, wakasema, “kweli mtu huyu alikuwa Mwana wa Mungu” (Lk 23:44-46; Mt 27:54).
W. Kabila langu, Nimekutendea nini? au kwa jambo gani nimekusikitisha? Nijibu !
1. Mimi nimekukomboa kutoka nchi ya Misri, nawe ukamtengenezea mkombozi wako msalaba.
2. Mimi nimewapiga mijeledi Wamisri kwa ajili yako, nakamtoa mkombozi wako apigwe mijeledi.
3. Mimi nimeifunua bahari ya Sham mbele yako, nawe ukaufunua ubavu wangu kwa mkuki.
4. Mimi nimekulisha mana na maji jangwani, nawe ukaninywesha nyongo na siki.
5. Mimi nimewapiga wafalme wa Kanaani kwa ajili yako, nawe ukanipiga kichwa changu kwa mwanzi.
6. Mimi nimekutukuza na kukuinua juu ya mataifa, nawe ukanitundika katika mti wa msalaba.
Kabila langu, Nimekutendea nini? au kwa jambo gani nimekusikitisha? Nijibu !
(Kutoka “Mashutumu ya Ijumaa Kuu, “Kabila langu”)
Tuombe: Bwana Yesu, tunatangaza kifo chako mpaka utakapokuja. Tunaomba tangazo hili liwafikie watu wote wasiokujua. Wote wakukiri wewe uliye hekalu jipya la kumwabudia Mungu. Wale wakutafutao katika kivuli wajalie Roho wako, waweze kukukiri kama wale wapagani “Hakika huyu alikuwa Mwana wa Mungu”. Amina
P. Ilikuwa yapata saa sita mchana; jua likaacha kuangaza, giza likaivamia nchi yote mpaka saa tisa, na pazia lililokuwa limetundikwa Hekaluni likapasuka katikati. Yesu akalia kwa sauti kubwa: “Baba, mikononi nwako naiweka roho yangu”. Alipokwisha kusema hayo, akatoa roho. Jemadari na wale waliokuwa wakimchunga Yesu walipoona mtetemeko wa ardhi na yale mambo yaliyotukia, wakaogopa sana, wakasema, “kweli mtu huyu alikuwa Mwana wa Mungu” (Lk 23:44-46; Mt 27:54).
W. Kabila langu, Nimekutendea nini? au kwa jambo gani nimekusikitisha? Nijibu !
1. Mimi nimekukomboa kutoka nchi ya Misri, nawe ukamtengenezea mkombozi wako msalaba.
2. Mimi nimewapiga mijeledi Wamisri kwa ajili yako, nakamtoa mkombozi wako apigwe mijeledi.
3. Mimi nimeifunua bahari ya Sham mbele yako, nawe ukaufunua ubavu wangu kwa mkuki.
4. Mimi nimekulisha mana na maji jangwani, nawe ukaninywesha nyongo na siki.
5. Mimi nimewapiga wafalme wa Kanaani kwa ajili yako, nawe ukanipiga kichwa changu kwa mwanzi.
6. Mimi nimekutukuza na kukuinua juu ya mataifa, nawe ukanitundika katika mti wa msalaba.
Kabila langu, Nimekutendea nini? au kwa jambo gani nimekusikitisha? Nijibu !
(Kutoka “Mashutumu ya Ijumaa Kuu, “Kabila langu”)
Tuombe: Bwana Yesu, tunatangaza kifo chako mpaka utakapokuja. Tunaomba tangazo hili liwafikie watu wote wasiokujua. Wote wakukiri wewe uliye hekalu jipya la kumwabudia Mungu. Wale wakutafutao katika kivuli wajalie Roho wako, waweze kukukiri kama wale wapagani “Hakika huyu alikuwa Mwana wa Mungu”. Amina
Comments
Post a Comment